
Ev. John Mafuru
0764736335
SOMO: JE,
MTU AKIFA ANAENDA WAPI?
KIFO
ni mgeni asiyezoeleka miongoni mwa binadamu wengi. Kila mtu anapofiwa na ndugu,
mke,mume jamaa na rafiki wa karibu huumia sana na wengine mpaka hukata tamaa ya
kuendelea kuishi na wengine huamua kujiua. Kifo huleta machungu sana katika
maisha ya mwanadamu na ni tokeo la dhambi iliyofanywa na wazazi wetu wa kwanza.
Imani nyingi zimeibuka zikizungumzia kifo kwa namna mbalimbali, Imani nyingine
zinaamini mtu akifa akiwa ametenda mambo mema moja kwa moja anakwenda mbinguni,
akifa amefanya matendo mabaya moja kwa moja anaenda motoni, Imani zingine
zinafundisha kuwa mtu akifa kama anadhambi ataombewa na viongozi wa dini naye
atasamehewa na kuingia mbinguni, zingine zinafundisha mtu akifa kama katenda
mema atazaliwa sehemu katika familia ya kitajiri au kifalme na kama katenda
mabaya atazaliwa katika familia duni au kiumbe kingine kama mjusi n.k. Imani
zingine zinafundisha mtu akifa anakuwa hai na ndugu au jamaa au watoto wanaweza
kuwasiliana nae wanapohitaji. Kwa ufupi kuna Imani nyingi sana kuhusu mtu
anapokufa anakwenda wapi.
Mpenmzi
msomaji usiogope kusikia hayo, sasa tukiulize kitabu kitakatifu (Biblia) je mtu
akifa hatima yake ni nini na anakuwa wapi. KIFO katika kamusi ya Oxford
imetafsiriwa kama “End of something” mwisho wa kitu fulani. Ili kupata ufafanuzi mzuri
kwanza tujue nini kinamfanya mtu kuwa HAI. Uhai ni Mwili jumlisha pumzi “Bwana
Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai, mtu
akawa nafsi hai”. Mwanzo 2:7. Tazama hii UHAI=Mavumbi+Pumzi. KIFO=Mavumbi-Pumzi
ya Uhai.
Katika
Mwanzo 2:7 tunapata maneno mawili nalo ni MWILI ambao ulitokana na mavumbi au ardhi na PUMZI
YA UHAI ambayo Mungu aliipulizia puani kwa mwanadamu akawa kiumbe hai. Baada ya
dhambi Mungu alisema maneno haya, Mwanzo 3:19 “kwa jasho la uso wako
utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa, kwa
maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi” akiwa na maana kwamba kwa kuwa
MWILI ni mavumbi basi anapokufa mtu mwili unarudi mavumbini ndio maana mtu
yoyote akifa lazima anazikwa chini ya ardhi na anaoza hukona kuwa udongo. Ayubu 27:3 inasema hivi “kwa kuwa uhai
wangu ukali mzima ndani yangu, na roho ya Mungu I katika pua yangu” inamaana
kuwa roho ni sawa na Pumzi ambayo Mungu aliipulizia puani mwa mwanadamu akawa
hai.
Kwa mwandamu kifo kina maana ni utengano kati ya
MWILI na PUMZI YA UHAI. Kunapokuwa na utengano huu hapo ndo mwisho wa mwanadamu
na katika ulimwengu huu kifo siku zote ni kipya hakizoeleki kabisa. Hebu
fuatana name katika mafungu haya ili kujifunza Zaidi.
Muhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia
nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa”. Hivyo mtu anapokufa
haendi popote bali mwili hurudi mavumbini na Mungu anaichukua Pumzi yake ya
uhai. Pia Muhubiri 9:5
inasema “kwaq sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa,lakini wafuhawajui
neon lolote,wala hawana ijara tena,maana kumbukumbu lao limesahauliwa”. Mtu
anapokufa habari zake zinaishia hapo hajui lolote wala hawezi fanya lolote
hivyo wale wenye Imani ya kwamba mtu akifa mnaweza kuongea nae Mungu wa
mbinguni ameshakuelimisha ya kwamba mtu akifa basi habari zatoweka. Soma pia Zaburi
115:17. Yesu kristo katika Yohana
11:11 na kuendelea alifananisha kifo na usingizi (kisa cha lazaro), chukulia
mfano ya kwamba ukilala je unakumbuka lolote au unajua kinachoendelea duniani.
Tumekwisha elewa kwamba mtu anapokufa mwili
unarudi mavumbini na roho au pumzi ya uhai uichukua Mungu aliyeipulizia. Je
nini kitafuata baada ya mtu kufa?. Kwasisi tulio hai tumaini tunalo ambalo
Mungu amelifununa kwetu kupitia manabii wake na mwanawe mpendwa Yesu kristo. Yohana 5:28-29 inasema hivi
Msistaajabie maneno hayo,kwa maana saa yaja ambayo watu wote waliomo makaburini
wataisikia sauti yake.Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima,
na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu, na hili jambo litatokea pale
yesu kristo atakapo kuwa anarudi mara ya pili hapa duniani ndipo wafu wote
watasikia parapanda ikilia waliokufa katika yesu watafufuliwa kwanza na kuvikwa
kutokufa soma pia 1Thesalonike 4:15, 16 na 1Korintho 15:51-54.
Ewe mpenzi msomaji usiwe na wasiwasi juu ya kifo
kwa maan atumaini lipo katika kristo yesu, Ufunuo 1:17-18 inasema “Nami
nilipomwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa.Akaweka mkonowake wa
kuumejuu yangu, akasema, usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho na aliye
hai;name nalikuwa nimekufa na tazama ni hai hata milele.Nami ninazofunguo za
mauti na za kuzimu.” Usomapo ujumbe huu njoo sasa kwa Yesu ,mshindi na aliye na
fungua za mauti ili uweze kuwa hai hata ukifa kwaa maana Yesu ndiye njia na
uzima.
Barikiwa mpenzi msomaji na usisite kuwasiliana
nasi kwa jambo lolote liwe swali au ufafanuzi wa mada Fulani au maoni na
ushauri.

Comments
Post a Comment